Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Juni 03, 2023 Local time: 21:21

Umoja wa Afrika Wasema Hautoruhusu Mauaji ya Halaiki Burundi


had carried out coordinated attacks on three military installations, Dec. 1

Umoja wa Afrika umesema hapo Alhamisi kwamba haupo tayari kuona yanatokea mauaji ya halaiki nchini Burundi.

Wakati umoja huo ukitoa tamko hilo, Umoja wa Mataifa imetoa amri ya kufanyika kwa uchunguzi wa vitendo vilivyosambaa vya unyanyasaji na kuonya kutokea kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Baraza la amani na usalama la Umoja wa Afrika limesema kupitia ujumbe wa Twitter wakati wanachama wakijadili hali ya Burundi.

Baraza hilo limedai kwamba Afrika haitoruhusu kutokea kwa mauaji mengine ya halaiki katika ardhi yake.

Mauaji yanayoendelea yamesababisha dunia kutaka kumalizwa kwa ghasia nchini Burundi ambapo watu zaidi ya 400 wameshakufa toka mwezi Aprili.

Hoja za uchochezi zimekuwa zikizidi na kuzusha hofu kwamba nchi hiyo inaweza ikakabiliwa na tukio kama lililotokea nchini Rwanda

XS
SM
MD
LG