Bodi ya filamu nchini Kenya imestushwa na kiwango kikubwa cha filamu ambazo wakazi wa pwani wanatizama japo hazijapitiwa na bodi hiyo.
Akizungumza na bodi ya Maimamu na wahubiri wa kiislam nchini Kenya (CIPK) pamoja na kamishna wa kaunti ya Mombasa Bw.Nelson Marwa, afisa wa bodi hiyo Bw. Ezekiel Mutua amesema wengi wanaodhulumiwa na uovu huu ni watoto na hivyo kusisitiza kuwa bodi hiyo imejiandaa kukabiliana na suala hilo.
Nyingi ya filamu hizo zinaingizwa nchini humo kupitia mpaka wa Kenya na Tanzania na sasa serikali ya Kenya kupitia bodi hiyo inalenga kukabiliana na swala hilo ambalo linawaweka vijana hatarini.
Kwani inadaiwa filamu hizo zinatumiwa kuendeleza utalii wa ngono na pia itikadi kali za kidini na ugaidi.