Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 04:26

Tanzania yaanza zoezi la kuhesabu watu .


Mkusanyiko wa watu nchini Tanzania
Mkusanyiko wa watu nchini Tanzania
Tanzania imeanza zoezi la kuhesabu watu siku ya jumapili kwa muda wa siku saba.

Awali zoezi hilo lilionekana kuwa na upinzani mkali kutoka katika taarifa za kidini lakini taarifa zinasema zoezi limeanza bila matatizo yoyote.

Watu waliohesababiwa wameeleza kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa maafisa wa sensa ambao walizunguuka katika makazi mbalimbali ya watu kutekeleza zoezi hilo.

Jijini dar es salaam mwandishi wetu George Njogopa aliyefuatilia zoezi hilo kwa karibu anasema aliwaona maafisa wakipita nyumba mbalimbali ili kutekeleza zoezi hilo ambalo hufanyika takriban kila baada ya miaka mitano au kumi.

Kutoka na mfumo wa utaratibu huu, ikiwa kuna Mtanzani aliyoko nje ya nchi basi hatopata fursa ya kuhesababiwa.
XS
SM
MD
LG