Fainali za kombe la mataifa Afrika zinaendelea katika hatua ya makundi na leo huku kukiwa na mechi mbili kundi C ambapo Gabon inachuana na Niger wakati Morocco inagongana na Tunisia, mechi hizo zote zinafanyika mjini Libreville, Gabon.
Katika mechi za kundi B Jumapili Ivory Coast ilipata ushindi wa 1-0 dhidi ya Sudan wakati Angola iliichapa Burkina Faso 2-1 katika mechi zilizochezwa Malabo, Equatorial Guinea. Jumanne Ghana ambao wamewahi kushinda kombe hilo mara nne wanachuana na Botswana katika mechi za kundi D na baadaye Mali dhidi ya Guinea katika kundi hilo.