Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 14:06

Wawili zaidi wahukumiwa kwa ugaidi


Watu wawili zaidi wamarekani wenye asili ya kisomali wamehukumiwa kwenda gerezani kwa kupanga njama za kutoa msaada wa vifaa kwa kundi la Islamic State.

Hanad Musse, mwenye umri wa miaka 21, ni mmoja kati ya marafiki tisa kutoka jumuiya kubwa ya Wasomali ya hapa Marekani, jimboni Minesota ambao walihukumiwa wiki hii kwa kupanga njama za kujiunga na kundi hilo la wanamgambo.

Mapema Jumanne, mmoja wa watuhumiwa wenzake, Hamza Ahmed, alihukumiwa miaka 15 jela katika makossa yanayo husiana na kupanga njama hizo.

Musse, Ahmed na wenzake wengina wawili, walisafiri kwenda New York mwezi Novemba m waka 2014, wakipanga kusafiri kwenda Ugiriki na baadaye kuingia nchini Syria.

Walikamatwa na maafisa usalama wa serekali kuu na kutolewa kwenye ndege.

XS
SM
MD
LG