Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 12:54

Mwanasiasa Zitto Kabwe avuliwa uwanachama


Zitto Kabwe aliyevuliwa uwanachama wa CHADEMA
Zitto Kabwe aliyevuliwa uwanachama wa CHADEMA

Chama cha upinzani cha Maendeleo na Demokrasia Chadema nchini Tanzania, kimemvua uanachama mbunge wa Kigoma kaskazini Zitto Kabwe baada ya mahakama kutupilia mbali kesi yake ya kupinga asijadiliwe na chama hicho.

Uamuzi huo umetangazwa Jumanne na mwanasheria mkuu wa chama hicho Tundu Lisu mara tu mahakama ilipomaliza kesi hiyo.

Zito Kabwe alikiburuza chama chake mahakamani baada ya kutaka kumjadili yeye na wanachama wengine wawili ambao tayari walifukuzwa mwaka jana kutokana na sababu za kimaadili .

Akizungumza na sauti ya Amerika mwanasheria wa chama Lisu, amesema katiba ya Chadema inakataza kiongozi au mwanachama yeyeto kukishitaki chama na endapo atabainika mtu kufanya hivyo hatua ya kwanza ni kumfuta uanachama.

Hatua hiyo imeleta hisia tofauti hasa ikizingatiwa kwamba nchini Tanzania inakaribiwa kufanyika uchaguzi mkuu baadae mwaka huu. Lakini Lisu amesema hakuna athari zozote zinazoweza kupatikana kutokana na uamuzi huo.

XS
SM
MD
LG