Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 27, 2024 Local time: 06:18

Mauaji ya kibaguzi yaendelea Bangladesh


Mtumishi wa dini ya Hindu wa Bangladesh alishambuliwa na kuuwawa Ijumaa asubuhi alipokuwa akitembea katika kile polisi wanachoamini kuwa mfululizo wa mashambulizi mabaya dhidi ya dini za wachache nchini humo.

Nityaranjan Pande, mwenye umri wa miaka 62, alikuwa akitembea katika eneo la wilaya ya kaskazini magharibi ya Pabna wakati watu wasiojulikana walipomshambulia na kumuuwa papo hapo.

Zaidi ya watu 40 wameuwawa katika mashambulzi kama hayo katika miaka mitatu iliyoopita na ghasia hizio zinmeongeeka katika miezi michache iliopita.

Padiri wa kihindu alishambuliwa na kuuwawa Jumanne akiwa njiani kwenda kwenye nyumba ya ibada.

XS
SM
MD
LG