Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 17, 2024 Local time: 14:47

Magenge yenye silaha yavunja Maktaba ya Taifa, UNESCO yalaani uharibifu wa taasisi za elimu


Ghasia zinazo endelea nchini Haiti.
Ghasia zinazo endelea nchini Haiti.

Maktaba ya Taifa ya Haiti imevunjwa na magenge yenye silaha yanayowatisha watu katika mji mji mkuu wa  Port-au-Prince kwenye taifa  hilo la Carribean, mkurugenzi wa maktaba hiyo ameiambia AFP, ambapo UNESCO imelaani mashambulizi kadhaa ya uharibifu katika taasisi za Elimu na Sanaa nchini humo.

Mkurugenzi wa Maktaba Dangelo Neard alisema kuwa historia ya Haiti – Ukanda wa Magharibi wa jamhuri ya pili kongwe – ilikuwa inatishiwa usalama wake.

“Mkusanyiko wa nyaraka zetu ziko hatarini. Tuna nyaraka ambazo ni nadra kupatikana za zaidi ya miaka 200, zenye umuhimu na turathi zetu, ambazo ziko hatarini kuchomwa moto au kuharibiwa na majambazi,” alisema.

“Niliambiwa kuwa wahuni hawa wanachukua samani za taasisi zetu. Pia wameiba jenereta la jengo hilo.”

Makundi yenye silaha yanadhibiti sehemu kubwa ya Port-au-Prince na maeneo ya pembeni mwa nchi kutokana na kukosekana kwa serikali inayofanya kazi na kuendelea kuchelewa kuundwa mamlaka ya mpito iliyoahidiwa.

Baada ya siku kadhaa za utulivu kiasi, mashambulizi yalirudi tena katika maeneo kadhaa ya jirani ya Port-au-Prince kuanzia Jumatatu.

Shambulizi hilo katika Maktaba ya Taifa limekuja baada ya mashambulizi kadhaa wiki iliyopita katika vyuo vikuu viwili, Ecole Normale Superieure na National School of Arts.

Forum

XS
SM
MD
LG