Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 28, 2024 Local time: 12:22

Katiba mpya Togo: Rais kuchaguliwa na wabunge


Rais wa Togo Faure Gnassingbé (katikati) alipopokelewa na rais wa Jumuiya ya Kiuchimi ya nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS). Picha na Kola Sulaimon / AFP
Rais wa Togo Faure Gnassingbé (katikati) alipopokelewa na rais wa Jumuiya ya Kiuchimi ya nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS). Picha na Kola Sulaimon / AFP

Bunge la Togo sasa yakabidhiwa mamlaka ya kumchagua Rais wa nchi hiyo ndogo ya Afrika Magharibi baada ya wabunge kupitisha katiba na kubadilisha mfumo wa nchi hiyo kutoka kwa utawala wa Rais kuelekea mfumo wa bunge.

Rais atachaguliwa bila mjadala na wabunge kwa muhula mmoja wa miaka sita", na sio na umma, kulingana na Katiba mapya.

Mabadiliko hayo yamefanyika chini ya mwezi mmoja kabla ya uchaguzi ujao wa wabunge, lakini bado haijajulikana ni lini mabadiliko hayo -- ambayo yalipitishwa kwa kura 89 za ndio, moja ya kupinga na moja kutopiga kura -- yataanza kutumika.

Hivi sasa, rais anaweza kuhudumu hadi mihula miwili ya miaka mitano, Mabadiliko ya katiba, yalipendekezwa na kundi la wabunge wengi wao kutoka chama tawala cha Union for the Republic (UNIR), yalipitishwa kwa karibu kwa kauli moja.

Upinzani nchini humo, ambao ulisusia uchaguzi uliopita wa wabunge mwaka wa 2018 na kushutumu "upungufu" katika zoezi la sensa ya wapiga kura, hauwakilishwi vyema katika bunge la kitaifa.

Katiba mpya pia inabuni nafasi ya mkuu wa baraza la mawaziri mwenye “mamlaka kamili ya kusimamia mambo ya serikali na kuwajibika ipasavyo.

Forum

XS
SM
MD
LG