Mtuhumiwa mwingine wa mauaji ya Kimbari akamatwa Uholanzi

Mamia ya watu wakipita mbele ya kanisa la Mubirizi, ambapo zaidi ya Watutsi 14,000 waliuawa wakati wa mauaji ya Kimbari ya Rwanda mwaka 1994. Picha na Clement DI ROMA / AFP.

Afisa wa jeshi wa zamani nchini Rwanda ambaye anashukiwa jukumu lake kubwa katika mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994 amekamatwa nchini Uholanzi siku ya Jumanne, waendesha mashtaka wa Uholanzi walisema.

Pierre-Claver Karangwa mwenye umri wa miaka 67, aliwekwa kizuizini nchini Uholanzi, kuchunguzwa jukumu lake katika mauaji ya kimbari, ambayo waendesha mashtaka walianza baada ya Mahakama ya juu ya Uholanzi mwezi Juni mwaka huu kusema haiwezi kumrejesha Rwanda mtuhumiwa huyo kwa kuhofia kutotendewa haki na mahakama.

Rwanda inamshutumu Karangwa kwa jukumu kubwa katika mauaji ya takriban Watutsi 30,000 katika parokia ya Mugina iliyoko jirani na mji mkuu wa Kigali, mwezi Aprili mwaka 1994 na aliomba kujisalimisha mwaka 2012.

Katika kesi mahakamani kuhusu uwezekano wa kurejeshwa mwezi Desemba 2022, Karangwa alisema hana hatia katika tuhuma hizo dhidi yake.

Karangwa, ambaye amekuwa akiishi Uholanzi tangu mwaka 1998, utaifa wake wa Uholanzi ulibatilishwa kutokana na tuhuma za mauaji ya halaiki, kinadharia kuandaa njia ya kurejeshwa Rwanda.

Lakini Mahakama ya Juu ilikanusha hili kwa sababu ya nafasi ya Karangwa kama mwanasiasa wa upinzani.

Waendesha mashtaka wa Uholanzi wamesema wanamshuku Karangwa kwa kushiriki kuchoma nyumba wakiwemo dazeni ya wanawake na watoto, kufuatia shambulio la parokia ya Mugina.

Takriban watu 800,000 wa kabila la Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda, yaliyoratibiwa na watu wenye msimamo mkali wa serikali ya Wahutu na kuwanyonga viongozi wa eneo hilo na raia.

Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP