Liz Truss ni Waziri Mkuu mpya wa Uingereza

FILE - Liz Truss akiwa katika ukumbi wa Wembley Arena, London, Aug. 31, 2022.

Truss na aliyekuwa Waziri wa Fedha Rishi Sunak walikuwa wanagombea nafasi hiyo ya juu katika chama.

Atapochukua madaraka, Truss atakuwa anakabiliwa na kudorora kwa uchumi wa Uingereza na kupanda kwa gharama za nishati.

Waziri Mkuu Boris Johnson alitangaza Julai kuwa ataachia madaraka baada ya serikali yake ilipokumbwa na kashfa, kama vile kuvunja baadhi ya kanuni za serikali yake za kudhibiti COVID-19.

Jumanne, Truss atasafiri kwenda Scotland, ambako Malkia Elizabeth atamkaribisha rasmi kuunda serikali.

Baadhi ya taarifa hii inatokana na mashirika ya habari ya AP na Reuters