Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 18:09

Zelenskyy atoa mwito wa kuundwa kikosi cha Ulaya


Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, ametoa wito wa kuundwa kikosi cha pamoja cha kijeshi cha Umoja wa Ulaya, akisema bara hilo lazima lijitegemee huku kukiwa na tishio la kudumu kutoka kwa Russia, na kutokuwa na uhakika kuhusu uungwaji mkono wa Marekani, hali aliyoielezea kama ukweli mpya.

“Lazima tujenge Vikosi vya Wanajeshi vya Ulaya ili mustakabali wa Ulaya utegemee watu wa Ulaya pekee na maamuzi kuhusu Ulaya yafanywe barani Ulaya,” Zelenskyy amesema katika hotuba yake kwenye Mkutano wa Usalama wa Munich, Februari 15.

Huku kukiwa na wasiwasi mjini Kyiv na Brussels kwamba wanaweza kutengwa katika juhudi za kukomesha uvamizi kamili wa Russia, dhidi ya Ukraine, na kusababisha makubaliano ya kuipendelea Moscow, amerejea tena kwamba Ukraine na Ulaya lazima zihusishwe katika mazungumzo yoyote.

Amesema Ukraine haitakubali kamwe mikataba nyuma ya migongo inayoihusu bila kushirikishwa.

Forum

XS
SM
MD
LG