Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 08:34

Zaidi ya waandamanaji 200 wakamatwa Brazil kufuatia uharibifu mkubwa kwenye mji wa Brasilia


Wafuasi wa rais wa zamani wa Brazil Jair Bolsonaro mjini Brasilia katika picha ya maktaba.
Wafuasi wa rais wa zamani wa Brazil Jair Bolsonaro mjini Brasilia katika picha ya maktaba.

Maafisa wa Brazil wamesema Jumatatu kwamba waekamata takriban wafuasi 200 wa rais wa zamani Jair Bolsonaro, ambao walifanya uvamizi  kwenye mahakama ya juu, bunge pamoja na makazi  ya rais Jumapili mjini Brasilia.

Video kutokana na matukio hayo zinaonyesha maelfu ya watu wakishambulia majengo ya serikali, wakivunja madirisha, kupanda kwenye mapaa pamoja na kufanya uharibifu. Serikali imesema kwamba washukiwa hao watawajibishwa kwa mujibu wa sheria baada ya uchunguzi kukamilika.

Waziri wa sheria Flavio Dino amesema pia kwamba serikali inafanya uchunguzi ili kufahamu ni nani aliyegharamia mamia ya mabasi yaliyowasafirisha waandamanji kwenda Brasilia. Wafuasi wa Bolsonaro wanataka arejeshwe madarakani, na kulitaka jeshi kufanya mapinduzi.

Bolsonaro aliondoka Brazil kabla ya kuapishwa kwa rais wa sasa Luiz Inacio Lula da Silva wiki moja iliyopita. Kiongozi huyo sasa anaishi kwenye jimbo la kusini mwa Marekani la Florida. Rais wa Marekani Joe Biden amekemea tukio hilo akisema ni la kushangaza.

XS
SM
MD
LG