Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 00:43

Wizi wa mafuta Nigeria wasababisha mgomo wa wafanyakazi


Mtambo haramu wa kusafishia mafuta Nigeria
Mtambo haramu wa kusafishia mafuta Nigeria

Wafanyakazi katika sekta ya petrol nchini Nigeria, wameitisha maandamano ya kitaifa kupinga wizi wa mafuta, hali ambayo imeathiri kwa kiasi kikubwa  uchumi wa nchi na mapato ya fedha za kigeni.

Umoja wa wafanya kazi wa petroli na gesi wa Nigeria, Pengassan, unasema majeshi ambayo yametumwa kwenye eneo la Niger Delta kulinda miundo mbinu na vinu vya petroli ndiyo kiini dhidi ya jitihada za kutokomeza wizi wa petroli.

Rais wa Umoja wa Pengassan, Festus Osifo anasema serekali ni lazima ichukue hatua madhubuti kwa wote wanaohusika kwenye wizi huo, unaorudisha nyuma maendeleo ya taifa. Ameongeza kusema kwamba wanajeshi na maafisa wa usalama wanaotumwa kulinda vituo vya petroli huko Niger Delta, wanashirikiana na wenyeji pamoja na wahalifu katika kuendeleza uovu huo.

Utafiti uliofanywa unaonyesha kuwa Nigeria inapoteza mapipa 700,000 ya mafuta kila siku na wala haijaweza kutoa mgao wa OPEC wa mapipa milioni 1.8 kila siku kama inavyohitajika.

XS
SM
MD
LG