Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 05:07

Waziri wa Ulinzi wa Ukraine asema kwamba mageuzi yanaendelea


Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Oleksii Reznikov alipohudhuria mkutano wa pamoja wa wanahabari, huku mashambulizi ya Russia dhidi ya Ukraine yakiendelea, mjini Kyiv, Ukraine Oktoba 26, 2022.
Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Oleksii Reznikov alipohudhuria mkutano wa pamoja wa wanahabari, huku mashambulizi ya Russia dhidi ya Ukraine yakiendelea, mjini Kyiv, Ukraine Oktoba 26, 2022.

Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Oleksii Reznikov alitweet Jumanne kwamba mageuzi yanaendelea, hata wakati wa vita, katika maoni ambayo yalikuja kati wa msururu wa kujiuzulu kwa watumishi wa  serikali na kufukuzwa kazi na uvumi kwamba angebadilishwa.

Asanteni nyote kwa msaada wenu, pamoja na ukosoaji wa kujenga. Tunatoa hitimisho, Reznikov alisema.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy hajazungumza hadharani kuhusu maoni kutoka kwa mbunge aliyependekeza Reznikov ahamishiwe wadhifa mwingine.

Katika hotuba yake ya kila siku Jumatatu, Zelenskyy alisema serikali yake inaimarisha nafasi zetu za usimamizi, ikiwa ni pamoja na kuwateua wasimamizi wenye uzoefu wa kijeshi katika mikoa ya mpaka na mstari wa mbele.

Reznikov amesema ingawa hana mpango wa kujiuzulu, uamuzi wowote kuhusu mustakabali wake utatolewa na rais.

XS
SM
MD
LG