Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 24, 2025 Local time: 00:23

Waziri wa ulinzi wa Indonesia ashinda urais


Waziri wa ulinzi wa Indonesia, Prabowo Subianto, aliyewahi kuwa mkosoaji mkubwa wa China, ameibuka na ushindi katika uchaguzi wa urais wa Indonesia

Wachambuzi wanasema hakuna uwezekano wa mabadiliko yoyote makubwa katika uhusiano wa mataifa ya Asia kusini mashariki na Beijing.

Hata hivyo, wasiwasi kuhusu usalama wa wafanyakazi na uchafuzi wa mazingira unaohusishwa na uwekezaji wa China, pamoja na madai ya Beijing, katika bahari ya South China, yatautia majaribuni uthabiti wa uhusiano huo.

Wakati rais Joko Widodo, alipokuwa madarakani, China imekuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Indonesia, ikitumia rasilimali zake tajiri.

Jokowi, kama anavyoitwa mara nyingi, ameitaka China, kuwekeza zaidi Indonesia na amekuwa mshirika mkuu katika mpango wake wa miundombinu wa BRI.

Forum

XS
SM
MD
LG