Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:47

Waziri wa Ulinzi wa Indonesia ajiandikisha kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa 2024


Mgombea urais Prabowo Subianto , Kushoto, na mgombea mwenza Gibran Rakabuming , kulia, baada ya kujiandikisha kushiriki zoezi hilo mwaka 2024.
Mgombea urais Prabowo Subianto , Kushoto, na mgombea mwenza Gibran Rakabuming , kulia, baada ya kujiandikisha kushiriki zoezi hilo mwaka 2024.

Waziri wa Ulinzi wa Indonesia Prabowo Subianto pamoja na mgombea mwenza ambaye ni mwana wa kiume wa rais wa taifa hilo Gibran Rakabuming Raka, Jumatano wamejiandikisha kushiriki kwenye uchaguzi wa rais mwaka ujao.

Zoezi hilo linatarajiwa kuwa na ushindani wa wagombea watatu, Subianto kamanda wa zamani wa jeshi akielezewa kuwa ana nafasi kubwa ya kushinda.

Karibu wakazi milioni 205 wa Indonesia, theluthi moja wakiwa vijana wa chini ya umri wa miaka 30, wanatarajiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo wa rais na bunge, utakaofanyika Februari 14 mwaka ujao, kwenye taifa hilo la tatu kwa ukubwa ulimwenguni.

Maelfu ya watu wamejitokeza Jumatano kumshangilia Prabowo mwenye umri wa miaka 72, na Raka wakati walipokuwa wakiwasilisha nyaraka zao pamoja na manifesto kwa maafisa wa uchaguzi katika mji mkuu wa Jakarta.

Forum

XS
SM
MD
LG