Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:50

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, atembelea Israel na Ukingo wa Magharibi


Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Antony Blinken, akiwa na waziri mkuu wa Palesta, Mahmoud Abbas wakiwa Ukingo wa Magharibi katika mji wa Ramallah, Januari 31, 2023.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Antony Blinken, akiwa na waziri mkuu wa Palesta, Mahmoud Abbas wakiwa Ukingo wa Magharibi katika mji wa Ramallah, Januari 31, 2023.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Antony Blinken, alitembelea eneo la katikati ya Israel na ukingo wa magharibi.

Katika ziara hiyo akitaka pande zote mbili kupunguza ghasia za karibuni, na kufanyia kazi kupatikana suluhisho la muda mrefu, lakini Marekani ilikuwa na wakati mgumu wa lengo lake la suluhisho la mataifa mawili.

Blinken alikutana na waziri mkuu wa Palestina, Mahmoud Abbas, Ramallah, baada ya mkutano wa mapema wa Jerusalem, na waziri wa ulinzi wa Israel, Yoav Gallant, ambaye ame-muhakikishia ahadi ya Marekani ya usalama kwa Usrael, kuwa ipo madhubuti.

Blinken aliahidi dola milioni 50 za usaidizi wa uchumi kwa Wapelestina kwa kipindi cha miaka miwili ijayo, juu ya msaada wa dola milioni 890 ulio ahidiwa awali, na huduma za kazi za simu za 4G katika ukingo wa magharibi.

XS
SM
MD
LG