Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 05:27

Waziri wa mambo ya nje wa China atetea Afrika ipewe kiti cha kudumu kwenye Baraza la usalama la UN


Waziri wa mambo ya nje wa China, Qin Gang na mwenyekiti wa tume ya AU Moussa Faki Mahamat, wakihudhuria uzinduzi wa kituo cha Afrika cha kudhibiti na kuzuia magonjwa( CDC Africa), mjini Addis Ababa, Jan 11, 2023
Waziri wa mambo ya nje wa China, Qin Gang na mwenyekiti wa tume ya AU Moussa Faki Mahamat, wakihudhuria uzinduzi wa kituo cha Afrika cha kudhibiti na kuzuia magonjwa( CDC Africa), mjini Addis Ababa, Jan 11, 2023

Waziri wa mambo ya nje wa China Qin Gang Jumatano amesema Afrika lazima iwe na sauti kubwa katika Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa na taasisi nyingine za kimataifa, ombi la muda mrefu la viongozi wa bara hilo.

Qin ametoa wito huo katika taarifa iliyotolewa wakati alipokutana na mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika ambaye alieleza kusikitishwa na kile alichosema ni kutengwa kwa Afrika katika utawala wa kimataifa.

“Tunapaswa kuongeza uwakilishi na sauti za nchi maskini, hasa za Afrika, katika Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa,” Qin alisema wakati wa uzinduzi wa makao makuu ya kituo cha Afrika cha kudhibiti na kuzuia magonjwa mjini Addis Ababa, kilichofadhiliwa na China.

Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Moussa Mahamat Faki amesema sio haki kuliona bara la Afrika halina kiti cha kudumu katika baraza kuu la dunia.

“Kwa miongo kadhaa sasa tumekua tukipambana kwa ajili ya mageuzi ya mfumo wa kimataifa kwa ujumla na hasa kwa niaba ya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa,” alisema.

XS
SM
MD
LG