Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 14:32
VOA Direct Packages

Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia akamatwa kutokana na tuhuma za ufisadi


Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia, Muhyiddin Yassin akiwasili kwenye ofisi za tume ya kupambana na ufisadi. March 9, 2023.
Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia, Muhyiddin Yassin akiwasili kwenye ofisi za tume ya kupambana na ufisadi. March 9, 2023.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Malaysia wamesema kwamba kukamatwa kwa waziri mkuu wa zamani Muhyiddin Yassin, Alhamisi hakushangazi , lakini ni jukumu la serikali kuonyesha kwamba kesi dhidi yake ambaye pia ni mpinzani mkubwa siyo wa kisiasa.

Muhyiddin alikamatwa kwenye makao makuu ya tume ya kupambana na ufisadi ya Malaysia, baada ya kujifikisha kwa mahojiano kuhusu kesi ya ufisadi inayoendelea dhidi yake.

Kupitia taarifa, tume hiyo imesema kwamba kiongozi huyo atafunguliwa mashtaka kadhaa Ijumaa, chini ya sheria za ufisadi kuhusiana na mradi wa Jana Wibawa unaohusishwa na mabilioni ya dola za kuwasaidia wakandarasi wa makabila ya Malay, pamoja na makundi mengine ya walio wachache, wakati wa janga la Covid-19. Waziri huyo zamani amekanusha madai hayo na badala yake kusema kwamba yana ushawishi wa kisiasa.

XS
SM
MD
LG