Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 18:18

Waziri mkuu wa Cambondia ageukia TikTok na Telegram baada ya kufungiwa Facebook


Waziri mkuu wa Cambodia Hun Sen. Phnom Penh, Cambodia, July 1, 2023.
Waziri mkuu wa Cambodia Hun Sen. Phnom Penh, Cambodia, July 1, 2023.

Tangu waziri mkuu wa Cambodia Hun Sen kufuta ukurasa wake wa Facebook mwishoni mwa mwezi  Juni ukiwa na wafuasi milioni 14, chama tawala cha Cambondian People’s Party kimekuwa kikiwshinikiza  wanafunzi pamoja na wafuasi watiifu  kumfuata kwenye majukwaa mengine.

Majukwaa mbadala ni kama vile Telegram na TikTok, lakini bado hakujakuwa na mabadiliko makubwa. Hun Sen alifuta ukurasa wake Juni 29 baada ya bodi inayosimamia Facebook na Instagram kutangaza kwamba alichochea ghasia na k hivyo kumfungia ukurasa huo kwa muda wa miezi 6.

Tangu wakati huo, Sen amekuwa akituma ujumbe wake kupitia Telegram ambako ana wafuasi 975,000 ikilinganishwa na 850,000 aliokuwa nao mwishoni mwa Juni. Akaunti yake mpya ya TikTok imejikuta ikiwa na takriban wafuasi 244,000, wakati pia akianza tena kutumia Twitter kwa mara ya kwanza baada ya mwaka mmoja.

Forum

XS
SM
MD
LG