Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 14:58

Waziri mkuu Truss akabiliwa na uasi ndani ya chama chake


Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss akitoka 10 Downing Street huko London Jumatano, Septemba 7, 2022.
Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss akitoka 10 Downing Street huko London Jumatano, Septemba 7, 2022.

Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss amekuwapo madarakani  kwa wiki sita pekee. Lakini tayari sera zake huru za kiuchumi zimesababisha mzozo wa kifedha, uingiliaji kati wa dharura wa benki kuu, Mageuzi kadhaa ya kurudi nyuma na kumfukuza kazi waziri wake wa fedha.

Sasa Truss anakabiliwa na uasi ndani ya Chama tawala cha Conservative ambao unaacha uongozi wake ukining'inia kwenye kamba. Mbunge wa kihafidhina Robert Halfon aliishutumu serikali hiyo Jumapili kwa kuichukulia nchi hiyo kama “panya wa maabara ambao wanaweza kufanyiwa majaribio ya juu ya soko huria."

Wahafidhina wanatafakari iwapo wajaribu kumfukuza kiongozi wao. Truss, wakati huo huo, amemteua waziri mpya wa Fedha , Jeremy Hunt, ambaye anapanga kubadili kwa kiasi kikubwa mpango wake wa kiuchumi atakapotoa taarifa ya bajeti Oktoba 31.

XS
SM
MD
LG