Wafanyakazi nchini Uingereza, Wales na Ireland ya Kaskazini, lakini sio Scotland watafanya mgomo tarehe 15 na tarehe 20 Disemba, baada ya chama chao cha Royal College Nursing ( RCN) kusema kwamba serikali imepinga ombi la mashauriano.
Hii itakuwa hatua ya hivi karibuni ya kusimamisha kazi nchini Uingereza ambapo mzozo wa miongo kadhaa wa mfumuko mkubwa wa bei na gharama kubwa ya maisha, umepelekea wafanyakazi katika sekta mbalimbali kudai nyongeza ya mishahara ili kumudu kupanda kwa bei za bidhaa za msingi.
Mkurungenzi wa chama hicho cha wauguzi (RNC) Patricia Marquis leo Ijumaa amewaomba radhi wagonjwa ambao wangefanyiwa upasuaji au matibabu, na kusema kuwa “ wauguzi wamesimama ili kutetea haki zao lakini muhimu zaidi kutetea haki za wagonjwa.”