Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:08

Watu wanne wauwawa katika mlipuko wa kujitoa muhanga Somalia


Mlipuko wa bomu Somalia
Mlipuko wa bomu Somalia

Polisi wa Somalia wamesema takriban watu wanne wameuwawa na mlipuko wa kujitoa mhanga uliolenga kituo cha ukaguzi karibu na uwanja wa ndege katika mji mkuu, Mogadishu.

Polisi wa Somalia wamesema takriban watu wanne wameuwawa na mlipuko wa kujitoa mhanga uliolenga kituo cha ukaguzi karibu na uwanja wa ndege katika mji mkuu, Mogadishu.

“Niliona watu wanne wamefariki kwenye eneo la tukio. Wawili kati yao walikuwa wanajeshi wa serikali waliofariki mara baada ya shambulio hilo,” alisema afisa wa polisi Ali Hassan.

Watu kadhaa waliojeruhiwa walichukuliwa kwenye gari la wagonjwa, kulingana na shahidi Hamdi Nur. Hakukuwa na maelezo juu ya majeruhi wengine.

Mlipuko huo ulitokea wakati wagombea urais walipokuwa wakielekea katika eneo la uwanja wa ndege kwenye ngome nyingi kuhutubia wabunge kabla ya kura ya Jumapili ya kumchagua rais.

Kundi la Kiislamu la Al-Shabab nchini Somalia lilidai kuhusika na shambulizi hilo ambalo liliharibu biashara ndogo ndogo kando ya barabara.

XS
SM
MD
LG