Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:13

Watu kadhaa wameuawa Iran kutokana na mashambulizi ya bunduki


Rais wa Iran Ebrahim Raisi akihutubia wafuasi wake nje ya uliokuw aubalozi wa Marekani mjini Tehran Nov. 4, 2022.
Rais wa Iran Ebrahim Raisi akihutubia wafuasi wake nje ya uliokuw aubalozi wa Marekani mjini Tehran Nov. 4, 2022.

Mtu aliyekuwa amejihami kwa bunduki amewaua watu watano na kujeruhi watu wengine 10 wakiwemo maafisa wa usalama katika mji wa Izeh, kusini magharibi mwa Iran.

Kati ya waliouawa ni mtoto wa kike na mwanamke.

Watu wengine ambao idadi yao haijatajwa, wakiwemo maafisa wa usalama, wamejeruhiwa.

Katika shambulizi ljngine, maafisa wawili wa kijeshi wamepigwa risasai na kuuawa katika mji wa Isfahan, nchini humo.

Shirika la habari la serikali ya Iran limeripoti kwamba waliotekeleza mashambulizi yote mawili walikuwa wanatumia usafiri wa pikipiki.

Haijabainika kilichopelekea mashambulizi hayo ama kama yanahusiana na maandamano yanayoendelea kote nchini Iran kwa muda wa miezi miwili sasa.

Makundi ya waandamanaji yalikuwa yamekusanyika katika sehemu tofauti za Izeh, wakipaaza sauti zenye ujumbe wa kupinga serikali, na kurushia polisi mawe, huku polisi wakitumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya.

XS
SM
MD
LG