Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 14:13

Watu 45 wameuawa Ufilipino kutokana na dhoruba Nalgae


Wafanyakazi wa uokozji wanawaondoa watu kwenye nyumba zao kufuatia mafuriko yaliyosababisha na dhoruba la kitropiki Nalgae (AFP Photo/Philippine Coast Guard)
Wafanyakazi wa uokozji wanawaondoa watu kwenye nyumba zao kufuatia mafuriko yaliyosababisha na dhoruba la kitropiki Nalgae (AFP Photo/Philippine Coast Guard)

Wataalamu wa hali ya hewa walisema Nalgae, iliyokuwa na upepo  wa kilomita 95  kwa saa, na upepo wa hadi kilomita 130 kwa saa, ulisababisha  maporomoko mengi ya ardhi  kwenye eneo la mashariki mwa Ufilipino

Dhoruba ya kitropiki Nalgae imeua watu wasiopungua 45 nchini Ufilipino. Mapema Jumamosi, shirika linalofuatilia majanga nchini humo lilisema kimbunga hicho kilisababisha vifo vya watu 72, lakini idadi hiyo ilipungua baada ya kukaguliwa na wafanyakazi katika eneo kwenye mikoa ya kusini na mashariki mwa nchi.

Wataalamu wa hali ya hewa walisema Nalgae, iliyokuwa na upepo wa kilomita 95 kwa saa, na upepo wa hadi kilomita 130 kwa saa, ulisababisha maporomoko mengi ya ardhi kwenye eneo la mashariki mwa Ufilipino.

Wakaazi wameshauriwa kuwa mafuriko na maporomoko ya ardhi yanaweza kutokea baada ya mvua kubwa ya Nalgae.

Meya wa Manila amefunga maeneo yote yenye makaburi kwenye jiji hilo kwa sababu Nalgae inakaribia wakati Wafilipino walipokuwa wanajitayarisha kuadhimisha “Siku ya Watakatifu Wote”-ALL SAINTS DAY kwa utamaduni wa kutembelea makaburi ya jamaa zao.

XS
SM
MD
LG