Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 05:38

Watu 22 wauawa katika shambulio la Russia kwenye kituo cha treni-Zelenskiy


Rais wa Ukraine akiwapongeza wanainchi wa Ukraine katika siku ya uhuru wa taifa, Agosti 24, Picha ya Reuters.
Rais wa Ukraine akiwapongeza wanainchi wa Ukraine katika siku ya uhuru wa taifa, Agosti 24, Picha ya Reuters.

Takriban watu 22 wameuawa na darzeni kujeruhiwa Jumatano katika shambulio la kombora la Russia kwenye kituo cha treni cha Ukraine, Rais Volodymyr Zelenskiy amesema, wakati taifa lake likiadhimisha uhuru wake kutoka kwa Moscow chini ya utawala wa Kisoviet

Zelenskiy alikuwa ameonya Jumanne juu ya hatari ya “uchokozi wa kuchukiza wa Russia” katika siku ya uhuru, ambayo kwa bahati imeadhimishwa miezi sita tangu vikosi vya Russia kuivamia Ukraine, na kuufanya mzozo huo kuwa mbaya zaidi barani Ulaya tangu vita vya pili vya dunia.

Katika hotuba yake kwa njia ya video kwa Baraza la usalama la Umoja wa mataifa, Zelenskiy amesema treni imeshambuliwa na roketi katika mji mdogo wa Chaplyne, umbali wa kilomita 145 magharibi mwa eneo linalokaliwa na Russia la Donetsk mashariki mwa Ukraine. Amesema mabehewa manne yaliteketea kwa moto.

“Chaplyne ni maumivu yetu leo. Kufikia sasa, kuna watu 22 waliokufa,” Zelenskiy amesema katika hotuba ya jioni, akiongeza kuwa Ukraine itaifanya Russia kuwajibika kwa kila kitu ilichofanya.

Hayo yakiarifiwa, Rais wa Marekani Joe Biden ametangaza msaada wa kijeshi wa dola bilioni 3 kwa Ukraine wakati nchi hiyo ikiadhimisha uhuru wake jana Jumatano, ukiwa msaada mkubwa wa Washington tangu uvamizi wa Russia miezi sita iliyopita, lakini msaada huo utachukua miezi au miaka kadhaa kabla ya kuwasili mjini Kyiv.

XS
SM
MD
LG