Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 19:13

Watu 19 wauwawa Nigeria


Kundi la wavulana wa shule wakisindikizwa na wanajeshi na maafisa wa Nigeria kufuatia kuachiliwa kwao baada ya kutekwa nyara wiki iliyopita, Ijumaa Desemba 18, 2020.
Kundi la wavulana wa shule wakisindikizwa na wanajeshi na maafisa wa Nigeria kufuatia kuachiliwa kwao baada ya kutekwa nyara wiki iliyopita, Ijumaa Desemba 18, 2020.

Watu wenye silaha wamewauwa wana usalama 19, wakiwemo wanajeshi 13, katika shambulio lililotokea kaskazini magharibi mwa jimbo la Kebbi, Nigeria, chanzo cha usalama na wakaazi walisema Jumatano.

Vita hivyo vilizuka Jumanne jioni huko Kanya, kijiji kilichopo wilaya ya Danko-Wasagu, siku moja tu baada ya darzeni ya wanamgambo wa kujilinda wenyewe kuuawa katika eneo moja.

Takriban walinzi 57 waliuawa katika eneo jirani la Sakaba siku ya Jumatatu katika shambulizi la kuvizia na magenge ya wahalifu waliokuwa na silaha nzito wanaojulikana kama majambazi.

Mamia ya watu wenye silaha walivamia Kanya, wakipambana na kikosi cha wanajeshi na polisi katika mapigano ya saa tatu, chanzo na wakaazi walisema.

Idadi ya waliouawa imefikia 19. Inajumuisha wanajeshi 13, polisi watano na mlinzi mmoja, afisa wa usalama, ambaye hakutaka kutajwa jina aliiambia AFP.

XS
SM
MD
LG