Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 14:10

Watoto zaidi waandikishwa kwenye magenge Haiti


Mkuu wa shirika la watoto la Umoja wa Mataifa, Jumatatu amesema kwamba watoto wanajumuisha takriban nusu ya wanachama wa makundi yenye silaha ya Haiti, na kutoa mwito wa kulindwa kwao.

Mkurugenzi mkuu wa UNICEF, Catherine Russel, ameuambia mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya watoto wa Haiti kwamba wanakadiria kuwa watoto wanachukuwa zaidi ya asilimia 50 ya wanachama wa magenge yenye silaha huku jumla ua idadi ya watoto wanao andikishwa na makundi hayo yameongezeka na kufikia asilimia 70 katika mwaka uliopita.

Ameongeza kusema wanatumika kama watoa taarifa, wapishi, watumwa wa ngono, na wanalazimishwa kuanzisha ghasia miongoni mwao.

Amesema magenge kwa kawaida huwauwa watoto na kwamba matukio ya unyanyasaji wa kingono kwa watoto yameongezeka maradufu mwaka huu kwa asilimia 1,000.

Forum

XS
SM
MD
LG