Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 06, 2025 Local time: 15:21

Wapiganaji wa Tigray wameondoka Afar


Moshi mkubwa baada ya shambulizi katika mji wa Mekelle, eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia. Okt 20, 2021. PICHA: AP
Moshi mkubwa baada ya shambulizi katika mji wa Mekelle, eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia. Okt 20, 2021. PICHA: AP

Wapiganaji wa Tigray wametangaza kujiondoa kabisa kutoka jimbo la Afar nchini Ethiopia.

Msemaji wa wapiganaji haoGetachew, ameambia shirika la habari la Reuters kwamba ana matumaini kwamba hatua yao itaruhusu msaada wa chakula, ambao unahitajika sana, utaingia Tigray kwa wingi.

Mkuu wa polisi wa Afar Ahmed Harif amesema kwamba wapiganaji hao wameondoka mji wa Abala, lakini bado wapo katika wilaya tatu za eneo hilo.

Amesema kwamba wapiganaji hao wanadhibithi barabara kuu kati ya Abala na mji mkuu wa Tigray wa Mekelle, akiongezea kwamba anaendelea kuzungumza na maafisa wa serikali katika sehemu hiyo pamoja na wapiganaji, wanaompatia taarifa zaidi.

XS
SM
MD
LG