Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 15:52

Wanamgambo wa JNIM wadai kuhusika na shambulio dhidi ya msafara wa Burkina Faso


Mwanajeshi wa Ufaransa akiwa amesimama ndani ya helikopta ya kijeshi wakati wa ziara ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa wanajeshi wa Operesheni Barkhane, wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu katika eneo la Sahel Afrika Magharibi mwaka 2017. (AP).
Mwanajeshi wa Ufaransa akiwa amesimama ndani ya helikopta ya kijeshi wakati wa ziara ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa wanajeshi wa Operesheni Barkhane, wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu katika eneo la Sahel Afrika Magharibi mwaka 2017. (AP).

Tawi la Al Qaeda lenye makao yake makuu Sahel, Jama'at Nusrat al-Islam wal Muslimeen (JNIM), limedai lilifanya shambulio dhidi ya msafara wa Burkina Faso ambao uliua zaidi ya wanajeshi kumi mwezi uliopita, Shirika la Ujasusi la SITE lilisema Jumanne.

Wanamgambo hao wa Kiislamu walishambulia msafara uliokuwa ukipeleka vifaa katika mji wa kaskazini mwa Burkina Faso mnamo Septemba 26, siku chache kabla ya nchi hiyo ya Afrika Magharibi kukumbwa na mapinduzi yake ya pili ya kijeshi mwaka huu.

JNIM ilidai kuhusika na shambulio hilo la kuvizia na kusema "ilisababisha hasara kubwa ya kiuchumi kwa adui na 'kusababisha mtikisiko' katika safu ya jeshi la Burkinabe, na kusababisha mapinduzi ya kijeshi", taarifa ya SITE ilisema.

Wanajeshi 11 walikutwa wamekufa na takriban raia 50 waliripotiwa kutoweka baada ya shambulio hilo, serikali iliyopita ilisema.

Hata hivyo, hati ya usalama wa ndani iliyopatikana na Reuters siku ya Jumanne ilitoa idadi ya vifo vya wanajeshi kuwa 27.

XS
SM
MD
LG