Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 01:55

Wanejeshi wa Ethiopia wanahusika mauaji ya waandamanaji


Kundi la haki za binadamu linasema wanajeshi wa usalama wa Ethiopia yamewaua zaidi ya watu 400 toka mwezi Novemba katika kupambana na waandamanaji katika jimbo la Oromia.

Oromiya, eneo la kusini la Ethiopia
Oromiya, eneo la kusini la Ethiopia

Katika ripoti mpya iliyotolewa, kundi la Human Rights Watch linasema wanajeshi wakifyatua mara kwa mara risasi za moto kwa waandamanaji wa Oromia baada ya kutoa onyo hafifu ama kutotoa kabisa huku wakati mwingine wakijaribu kutumia njia na juhudi za kutawanya mkusanyiko bila kuhatarisha maisha.

Taarifa imeeleza kwamba wengi wa wale waliouwawa walikuwa wanafunzi ikijumuisha watoto walio chini ya miaka 18.

Kundi hilo la haki za binadamu pia limesema polisi wamewakamata watu elfu kumi toka maandamano yaanze, na wengi wanashikiliwa bila kushitakiwa ama bila kuwa na fursa ya wanasheria na wana familia.

XS
SM
MD
LG