Wanamgambo wameuwa wanajeshi 17 wa Mali na raia wanne katika shambulio karibu na mji wa Tessit siku ya Jumapili, jeshi la Mali lilisema.
Wanajeshi tisa pia wameripotiwa kupotea na magari na vifaa viliharibiwa, ilisema katika taarifa iliyotolewa Jumatatu jioni, na kuongeza kuwa inashuku kuwa ni fuasi washirika wa kundi la Islamic State.
Tarehe 7 Agosti mwaka huu vitengo vya jeshi vya Tessit vilijibu kwa nguvu shambulio la hali ya juu na lililoratibiwa na vikundi vya kigaidi vilivyojihami, pengine kutoka kwa ISGS ((Islamic State in the Greater Sahara) na kunufaika na msaada wa ndege zisizo na rubani na mizinga, taarifa hiyo ilisema.