Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 17:12

Wanajeshi 14 nchini Mali wauwawa


Wanajeshi wa Mali wakipiga doria na askari kutoka kikosi cha Takuba karibu na mpaka wa Niger katika Mzingo wa Dansongo.REUTERS
Wanajeshi wa Mali wakipiga doria na askari kutoka kikosi cha Takuba karibu na mpaka wa Niger katika Mzingo wa Dansongo.REUTERS

Wanajeshi 14 wa Mali waliuawa na 11 kujeruhiwa siku ya Jumanne katika mashambulizi mawili tofauti katikati mwa Mali baada ya magari yao kukanyaga vilipuzi, jeshi lilisema Jumatano.

Matukio hayo yametokea katika mikoa ya kati ambapo wanamgambo wenye uhusiano na al Qaeda na Islamic State huwashambulia mara kwa mara raia, wanajeshi wa Mali, walinda amani wa Umoja wa Mataifa na vikosi vingine vya kimataifa.

Kutumwa kwa vikosi hivyo vya kujibu mashambulizi ya hivi karibuni kulisababisha kuuawa kwa wanamgambo 31, jeshi lilisema katika taarifa yake.

Reuters haikuweza kuthibitisha kwa uhuru ripoti hiyo na hakuna kundi lolote ambalo limedai kuhusika na mashambulizi hayo.

XS
SM
MD
LG