Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Julai 13, 2025 Local time: 05:11

Wanafunzi waitoroka Kyrgyzstan baada ya makazi yao kushambuliwa


Wanafunzi na raia wa Pakistani wakisubiri ndege kuondoka Kyrgyzstan, Mei 23, 2024. Picha na REUTERS/Vladimir Pirogov
Wanafunzi na raia wa Pakistani wakisubiri ndege kuondoka Kyrgyzstan, Mei 23, 2024. Picha na REUTERS/Vladimir Pirogov

Wanafunzi kutoka Pakistani na nchi nyingine za Asia wanaondoka Kyrgyzstan baada ya kundi la watu wenye hasira kushambulia makazi yao mwezi huu, ingawa wengine wanatumai kurejea hali itakapotulia.

Mamia ya vijana wa Kyrgyz walivamia makazi ya wanafunzi katika mji mkuu Bishkek mapema Ijumaa na kuwashambulia wanafunzi wa kigeni.

Polisi, ingawa walikuwapo, hawakuweza kuzuia vurugu hizo.

Serikali ya Pakistani imepanga safari za ndege za ziada kuondoka kila siku kutoka Bishkek na wanafunzi wengi wanatumia fursa hiyo kurejea nyumbani, angalau kwa muda.

Serikali ya Kyrgyzstan imejaribu kuwaondoa hofu wanafunzi wa kigeni na kufanya mikutano na viongozi wao, alisema Yousaf, ambaye alionyesha matumaini kwamba wale wanaoondoka watarejea baada ya miezi michache.

Polisi inawashikilia watu zaidi ya kumi wanaoshukiwa kuhusika na mashambulizi.

Forum

XS
SM
MD
LG