Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 18, 2025 Local time: 16:13

Wamarekani walelezea wasiwasi wao kuhusu namna demokrasia inavyoendeshwa nchini


Bango linaloitisha demokrasia kwenye mitaa ya Marekani.
Bango linaloitisha demokrasia kwenye mitaa ya Marekani.

Wamarekani hawafurahishwi na jinsi demokrasia inavyofanya hivi sasa.  Kwa mujibu ya ukusanyaji maoni uliofaywa na Shirika la habari la Asociated Press na kituo cha utafiti wa masuala ya umma NORC,  takriban asilimia 49 ya wamarekani wanasema demokrasia haifanyi kazi vizuri nchini Marekani.

Ni asilimia 10 pekee wanasema demokrasia inafanya kazi vizuri sana, wakati asilimia 40 wanasema kwamba inafanya kazi kiasi. Vyama vikuu viwili vya siasa nchini Marekani- vyote vilipata alama za chini kwa namna vinavyoendesha misingi ya demokrasia.

Asilimia 47 ya watu waliohojiwa walisema kwamba wademokrat wanafanya kazi isiyoridhisha katika kudumisha demokrsia, wakati asilimia 56 wakisema kwamba warepablikan wanahitaji kufanya vizuri zaidi.

Shirika la AP linasema kwamba ukusanyaji maoni unaonyesha kuna migawanyiko mikubwa ya kisiasa, wakati taifa likijikwamua kutokana na janga la corona pamoja na mfumuko wa bei na hofu ya kudorora kwa uchumi. Takwimu hizo zilikusanywa kati ya Juni 22 na 26 mwaka huu.

Forum

XS
SM
MD
LG