Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 01:53

Walinda amani watatu wa Senegal wa kikosi cha UN nchini Mali wauawa katika mlipuko


Walinda amani wa Senegal wa kikosi cha Umoja wa mataifa nchini Mali (MINUSMA), Mei 30, 2018. Picha ya AFP
Walinda amani wa Senegal wa kikosi cha Umoja wa mataifa nchini Mali (MINUSMA), Mei 30, 2018. Picha ya AFP

Walinda amani watatu wa Senegal wa kikosi cha Umoja wa mataifa nchini Mali waliuawa Jumanne wakati msafara wao ulipokanyaga bomu lililotegwa kando ya barabara katika eneo la katikati mwa Mali ambako wanamgambo wa kiislamu hufanya mashambulizi yao, Umoja wa mataifa umesema.

“Msafara wa kikosi cha MINUSMA ulikanyaga bomu la kujitengenezea,” MINUSMA imesema kwenye Twitter na kutoa idadi ya awali ya wanajeshi watatu waliofariki na wengine watano kujeruhiwa vikali.

Mali inakabiliwa na uasi wa miaka 11 wa wanamgambo wa kiislamu ambao umeua maelfu ya watu na kulazimisha maelfu ya wengine kuhama makazi yao.

Afisa wa Umoja wa mataifa ambaye hakutaka jina lake litajwe amethibitisha kwamba walinda usalama hao walikuwa wa kikosi cha Senegal kinachoshiriki kwenye tume ya MINUSMA.

XS
SM
MD
LG