Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Januari 19, 2025 Local time: 07:41
VOA Direct Packages

Wakimbizi wa Rohingya waliyopo Bangladesh kuanza kurejea Myanmar mwezi ujao


Wakimbizi wa Rohingya kwenye kambi moja ya wakimbizi nchini Bangladesh
Wakimbizi wa Rohingya kwenye kambi moja ya wakimbizi nchini Bangladesh

Wakimbizi wa Rohingya wamesema Jumatano kwamba wana mashaka iwapo Myanmar na nia ya dhati ya kuwakaribisha  nyumbani kwao, baada ya msemaji wa uongozi wa kijeshi nchini humo kusema kwamba wataanza kukaribisha kundi hilo  la walio wachache kuanzia mwezi ujao.

Ujumbe wa maafisa 17 kutoka kundi la kijeshi linalotawala Myanmar umetembelea Bangladesh wiki hii ili kufanya mahojiano na baadhi ya wakimbizi, ambao huenda wakarejea, ikiwa miaka 5 baada ya kufanyika msako mkali wa kijeshi uliopelekea idadi kubwa ya kabila la Rohingya kutoroka makwao.

Ziara hiyo iliyoongozwa na China na kufadhiliwa na Umoja wa Mataifa inaashiria kuanza kwa makubaliano kati ya Maynmar na Bangladesh, ya kuwerejesha wakimbizi baada ya muda mrefu wa wasiwasi kwamba wangeteseka iwapo wangerejea makwao.

Hata hivyo baadhi ya wa Rohingya waliohojiwa na wajumbe hao wameambia shirika la habari la AFP kwamba hawakupata majibu ya kuridhisha kuhusu haki zao za uraia wa Myanmar.

XS
SM
MD
LG