Mkutano wa Jumatatu unatayarisha njia kuelekea duru mpya ya mazungumzo ya Umoja wa Mataifa yatakayofanyika Misri baadaye mwakani.
Kikao hicho pia ni mtihani kuona dhamira ya mataifa katika kukabiliana na matatizo yakiwemo mabadiliko ya hali ya hewa, mizozo ya kisiasa ya kikanda. umwagikaji wa damu Ukraine pamoja na kupanda kwa bei za vyakula ulimwenguni.
Wakati akiomba ushirikiano wa kimataifa, mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa anayeondoka Patricia Espinosa amewambia wajumbe kwamba, "siyo vyema kusema kwamba sote tunapitia nyakati ngumu.
" Ni lazima tuelewe kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yanaendelea kutokea kwa kasi kubwa, na tunahitaji kuongeza kasi ya mashauriano." amesema Espinosa.