Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 01:20

Wafanyakazi wa mafuta Nigeria wamwomba Rais Tinubu kupeleka wanajeshi zaidi kukabiliana na wizi wa mafuta


Rais wa Nigeria Bola Tinubu akiangalia baada ya hafla ya kuapishwa kwake Abuja, Nigeria Mei 29, 2023. REUTERS.
Rais wa Nigeria Bola Tinubu akiangalia baada ya hafla ya kuapishwa kwake Abuja, Nigeria Mei 29, 2023. REUTERS.

Muungano wa wafanyakazi wa mafuta nchini Nigeria umemwomba Rais Bola Tinubu kupeleka wanajeshi zaidi ili kukabiliana na wizi wa mafuta na

Wizi mkubwa wa mafuta kutoka kwenye mabomba na visima umekuwa mojawapo ya changamoto kubwa za Tinubu katika miaka ya hivi karibuni, kupoteza fedha za serikali na kupunguza pato na mauzo ya nje ya nchi.

Nigeria, mzalishaji mkubwa wa mafuta barani Afrika, inategemea bidhaa hiyo kwa zaidi ya theluthi mbili ya mapato yake na takriban asilimia 90 ya mapato ya fedha za kigeni. Imepata shida kuongeza pato kwani wizi na hujuma zimewalazimu kampuni kuu za mafuta ikiwa ni pamoja na Shell na Exxon Mobil kuondoa mali zao katika eneo la pwani.

Pato la mafuta lilifikia mapipa milioni 1.48 kwa siku mwezi Februari, kwa mujibu wa data kutoka Shirika la Nchi zinazouza Petroli (OPEC). Ingawa uzalishaji wa mafuta unaimarika hatua kwa hatua, bado uko chini ya lengo la bajeti la mapipa milioni 1.78 kwa siku.

Forum

XS
SM
MD
LG