Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 30, 2024 Local time: 09:20

Wachimba madini wote waliokwama Zimbabwe waokolewa


Watu wakiwa karibu na mgodi iliyopo karibu na mji wa Kadoma Zimbabwe. Picha ya maktaba.
Watu wakiwa karibu na mgodi iliyopo karibu na mji wa Kadoma Zimbabwe. Picha ya maktaba.

Timu za waokozi nchini Zimbabwe Jumapili zimewatoa wachimba migodi wadogo 15 waliokwama chini ya ardhi kwenye mgodi wa Redwing, baada ya mapromoko ya ardhi siku ya  Alhamisi, msemaji wa serikali Nick Mangwana amesema Jumatatu.

Wachimbaji hao walikwama baada ya mkasa huo kutokea kwenye mgodi uliopo takriban kilomita 270 mashariki mwa mji mku wa Harare. Mangwana ameongeza kusema kwamba wachimbaji wote waliokwama wameokolewa, ingawa operesheni hiyo ilicheleweshwa kutokana ardhi isiyo imara, kulingana na kampuni ya Matallon Gold, inayomiliki mgodi wa Redwing.

Video iliorushwa kwenye mtandao wa X na Mangwana inawaonyesha wachimba madini hao wakiwa wamefunikwa na matope, huku wakishangiliwa na kundi dogo la watu, karibu na eneo la tukio.

Forum

XS
SM
MD
LG