Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 09:48

Waandishi wawili wa habari wamepokea vitisho nchini Uingereza


Nembo ya CPJ, kamati ya kuwatetea waandishi wa habari
Nembo ya CPJ, kamati ya kuwatetea waandishi wa habari

Volant Media, kituo cha utangazaji chenye  makao yake London cha kituo cha televisheni cha Kimataifa cha Iran, kilisema katika taarifa kwamba waandishi wake wawili wamepokea

Waandishi wawili wa habari wa Uingereza wenye asili ya Iran wanaofanya kazi nchini Uingereza kwa kituo huru cha lugha ya Farsi wamepokea vitisho "vya kuaminika" vya kuuawa kutoka kwa vikosi vya usalama vya Iran, shirika la utangazaji la kituo hicho limesema Jumatatu.

Volant Media, kituo cha utangazaji chenye makao yake London cha kituo cha televisheni cha Kimataifa cha Iran, kilisema katika taarifa kwamba waandishi wake wawili wamepokea "vitisho vya kuuawa kutoka kwa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu," wakiita hii ni "kuongezeka kwa hatari" kwa majaribio ya kukandamiza vyombo huru vya habari.

"Hivi ni vitisho vinavyofadhiliwa na serikali kwa waandishi wa habari nchini Uingereza," msemaji wa Volant Media alinukuliwa akisema.

Walinzi wa Mapinduzi "hawawezi kuruhusiwa kunyamazisha vyombo huru vya habari nchini Uingereza," aliongeza.

XS
SM
MD
LG