Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 20, 2024 Local time: 12:12

Vita Vya Israel- Hamas: Wanajeshi kumi wa Israel wauawa


Wanajeshi wa Israel wakijiandaa kuingia Ukanda wa Gaza Desemba 13,2023. Picha na REUTERS/Ronen Zvulun
Wanajeshi wa Israel wakijiandaa kuingia Ukanda wa Gaza Desemba 13,2023. Picha na REUTERS/Ronen Zvulun

Jeshi la Israel siku ya Jumatano limetangaza vifo vya wanajeshi wake kumi waliouawa katika mapigano kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, wakati walipokuwa wakifanya kampeni ya kuliangamiza kundi la wanamgambo wa Hamas.Jeshi la Israel limesema limeshambulia zaidi ya malengo 250 jana.

Wakati ya operesheni huko Gaza, majeshi ya Israel yaliipata miili ya watu wawili walikuwa wamechukuliwa mateka wakati Hamas walipoivamia Israel mwezi Oktoba, kitendo ambacho kililifanya jeshi la Israel kujibu.

Msemaji wa jeshi la ulinzi la Israel alisema Hamas ilikuwa ikiwashikilia mateka chini ya ardhi katika maeneo yenye msongamano mkubwa huko Gaza, na kufanya jitihada za uokoaji kuwa ngumu, lakini amesema Israel haitatetereka katika azma yake ya kumuachilia huru kila mateka.

Mapigano hayo yanayoendelea yamekuja wakati maonyo mapya yametolewa kuhusu athari za vita kwa raia wa Palestina huko Gaza.

“Hatahivyo, janga kubwa, tunalotegemea kuliona ni vifo zaidi vya raia na mateso, , na kuongezeka kwa ukosefu wa makazi ambako kunalitishia eneo hilo,” mkuu wa wakimbizi wa U.N, Filippo Grandi alisema Jumatano.

Papa Francis kwa mara nyingine tena maetoa wito wa kutaka sitisho la haraka la mapigano, wakati akitaka usambazaji wa misaada ya kibinadamu kwenda Gaza na kuachiliwa kwa mateka wanaoshikiliwa na Hamas.

Ikiwa ni dalili kuwa Marekani inazidi kuwa na wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa kiwango cha vifo vya raia kutokana na kampeni ya jeshi la Israel huko Gaza, Rais Joe Biden alimkemea hadharani waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu siku ya Jumanne, pamoja na kuwa bado anaiunga mkono kwa dhati Israel.

Forum

XS
SM
MD
LG