Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 12:47

Viongozi wa Guyana na Venezuela wakutana ili kupunguza taharuki


Rais wa Venezuela Nicolas Maduro (Kushoto) akitemba ma waziri Mkuu wa Saint Vincent and the Grenadines Ralph Everard Gonsalves muda mfupi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Argyle International Airport Alhamisi.
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro (Kushoto) akitemba ma waziri Mkuu wa Saint Vincent and the Grenadines Ralph Everard Gonsalves muda mfupi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Argyle International Airport Alhamisi.

Viongozi wa Venezuela na Guyana Alhamisi wanakutana kwenye kisiwa cha Caribbean cha St Vincent na Grenadines kwa mkutano wa kina, wakati wakijaribu kuzima taharuki za kieneo za muda mrefu.

Hali hiyo imeongezeka katika siku za karibuni baada ya wa Venezuela kupiga kura ya maoni inayodai theluthi mbili ya eneo la Guyana.

Kutokana na shinikizo la viongozi wa kieneo, rais wa Guyana Irfaan Ali na mwenzake wa Venezuela Nicolas Maduro wamekubaliana kukutana kwenye uwanja wa kimataifa wa Argyle kwenye kisiwa hicho kilichoko mashariki mwa Caribbean cha St Vincent.

Mawaziri wakuu wa Barbados, Dominica na Trinidad and Tobago pia wamesema kwamba watahudhuria kikao hicho. Ali aliwasili kwanza akifuatiwa na Maduro, aliyezungumza na wanahabari kwanza kabla ya kuanza kwa kikao chao.

Forum

XS
SM
MD
LG