Idara ya dharura imesema kwamba vifo vingi vilisababishwa na mafuriko baada ya mvua za siku mbili kuvuruga sherehe za Krismasi, na kupelekea zaidi ya wakazi 45,000 kuchukua hifadhi kwenye vituo maalum.
Picha kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha timu za uokozi zikiwasaidia wakazi waliokwama kwenye mafuriko, huku baadhi ya barabara zikiwa zimefungwa kutokana na hali hiyo.
Carmelito Heray anayeongoza timu ya dharura kwenye mji wa Clarin uliopo jimbo la Misamis Occidental ameiambia radio ya DZBB kwamba operesheni za uokozi zinaendelea wakati pia wakikadiria hasara iliyokea kwenye sekta ya kilimo.
Mifugo kama vile ng’ombe, mbuzi na kuku wanasemekana kuangamia pia kutokana na mafuriko.
Facebook Forum