Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:39

Utawala wa Biden unataka uwepo wa kanuni zaidi za kuzuia udukuzi


Biden
Biden

Utawala wa rais wa Marekani, Joe Biden, unasisitiza kuwepo kwa kanuni za kina zaidi za serekali kuu ili kufanya eneo la mtandao kuwa salama dhidi ya wadukuzi.

Hii ikiwa ni pamoja na kuhamisha majukumu ya usalama wa mtandao kutoka kwa watumiaji hadi kwa tasnia na kukabiliana na udukuzi ikiwa kama tishio la usalama wa taifa.

Mpango huo ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa mtandao ambao utawala ulitoa Alhamisi, ukionyesha malengo ya masafa marefu jinsi watu binafsi, serikali na wafanyabiashara wanaweza kufanya kazi kwa usalama katika ulimwengu wa kidijitali.

Hii ni pamoja na kuweka majukumu kwenye sekta ya utengenezaji wa programu za kompyuta zilizo salama ambazo zimeundwa kimakusudi, ili kupunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya dosari zinazoweza kutumiwa kabla ya kuletwa kwenye soko.

XS
SM
MD
LG