Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 10, 2024 Local time: 11:30

Upigaji kura waanza Senegal


Mgombea urais Bassirou Diomaye Faye, anayeungwa mkono na kiongozi wa upinzani wa Senegal Ousmane Sonko, akikusanya karatasi za kura katika kituo cha Ndiaganiao huko Mbour, Senegal Machi 24, 2024. REUTERS/Abdou Karim Ndoye
Mgombea urais Bassirou Diomaye Faye, anayeungwa mkono na kiongozi wa upinzani wa Senegal Ousmane Sonko, akikusanya karatasi za kura katika kituo cha Ndiaganiao huko Mbour, Senegal Machi 24, 2024. REUTERS/Abdou Karim Ndoye

Upigaji kura ulianza  nchini Senegal siku ya Jumapili katika uchaguzi wa rais uliocheleweshwa unaofanyika wakati kuna hali mbaya ya kisiasa ambayo imesababisha maandamano ya kupinga serikali na kuongeza uungwaji mkono kwa upinzani.

Upigaji kura ulianza nchini Senegal siku ya Jumapili katika uchaguzi wa rais uliocheleweshwa unaofanyika wakati kuna hali mbaya ya kisiasa ambayo imesababisha maandamano ya kupinga serikali na kuongeza uungwaji mkono kwa upinzani.

Hatarini ni uwezekano wa mwisho wa utawala ambao umesukuma sera rafiki kwa wawekezaji lakini ukashindwa kupunguza matatizo ya kiuchumi katika mojawapo ya demokrasia imara zaidi Afrika Magharibi inayokabiliwa na mapinduzi wakati tu inapokaribia kuwa mzalishaji mkubwa wa hivi karibuni wa mafuta na gesi wa bara hilo.

Kuna wagombea 19 wanaowania kuchukua nafasi ya Rais Macky Sall, ambaye anajiuzulu baada ya muhula wa pili uliokumbwa na machafuko kutokana na kufunguliwa mashitaka kwa kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko na wasiwasi kwamba Sall alitaka kurefusha mamlaka yake kupita ukomo wa katiba.

Mgombea huyo hayumo kwenye sanduku la kura kwa mara ya kwanza katika historia ya Senegal. Muungano wake tawala umemchagua waziri mkuu wa zamani Amadou Ba, mwenye umri wa miaka 62, kama mgombea wake.

Forum

XS
SM
MD
LG