Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Februari 12, 2025 Local time: 07:13

UN yataka ushirikiano zaidi wa Iran, kuhusu nyuklia


Chombo ya Umoja wa Mataifa cha uangalizi wa nguvu za Atomiki chenye nchi wanachama 35, Alhamisi kimepitisha azimio kwa mara nyingine kikiitaka Iran, kwa haraka kuboresha ushirikiano na chombo hicho.

Vilevile kimetaka kutolewa kwa ripoti ya kina kuishinikiza Iran kuingia katika mazungumzo maya ya nyuklia.

Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, na Marekani, ambazo zimeweka azimio hilo, zimepuuzia hatua za nyakati za mwisho za Iran ambazo wanaziona zisizo ya maana na ukweli za kupunguza kiwango chake cha Uranium ambacho kipo karibu kutengeneza silaha.

Wanadiplomasia wamesema hatua ya Iran ilikuwa ya makusudi katika kuondoa azimio hilo. China, Russia, na Burkina Faso zilipiga kura kupinga azimio wanadiplomasia waliokuwepo kwenye mkutano wamesema.

Nchi 19 zilipiga kura kuunga mkono, lakini 12 hazikushiriki upigaji kura huo.

Forum

XS
SM
MD
LG