Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 02:46
VOA Direct Packages

UN yasema Idadi ya watoto wanaopokea chakula cha bure shuleni imeongezeka ulimwenguni


Watoto wakisubiri msaada wa chakula nchini Ethiopia.
Watoto wakisubiri msaada wa chakula nchini Ethiopia.

Ripoti ya Jumanne kutoka shirika la Chakula Duniani ya Umoja wa Mataifa WFP imesema kwamba karibu watoto milioni 420 kote ulimwenguni walinufaika na chakula cha bure shuleni mwaka jana.

Hatua hiyo ni muhimu katika kukabiliana na viwango vya juu vya njaa vinavyoendelea kushuhudiwa kote ulimwenguni. Mkuu wa program ya chakula kwa watoto wa shule kutoka WFP, Carmen Burbano, amesema kwamba serikali kote ulimwenguni zinaonekana kutambua umuhimu wa lishe bora kwa watoto kama suala linalohitajika kupewa kipaumbele licha ya janga linaloshuhudiwa kote ulimwenguni na hasa kwenye mataifa masikini.

Ripoti hiyo imeongeza kusema kwamba idadi ya watoto wanaofikiwa na chakula kupitia program hiyo imepita ile ya kabla ya janga la Covid-19. WFP imesema kwamba mwaka jana, watoto milioni 418 kote ulimwenguni walipokea chakula shuleni, likiwa ongezeko la watoto milioni 30 kulinganishwa na mwanzoni mwa 2020.

XS
SM
MD
LG