Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 20, 2023 Local time: 19:54
VOA Direct Packages

UN yaonya kuhusu hatari ya kuongezeka kwa maji ya bahari katika miaka ya karibuni


Katibu mkuu wa UN Antonio Guterres

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema Jumanne kwamba viwango vya maji ya bahari vimepanda kwa haraka tangu 1900 na kuhatarisha baadhi ya mataifa ulimwenguni.

Baadhi ya mataifa hayo ni kama vile Bangladesh, China, India na Uholanzi yambayo yapo kwenye hatari ya kusombwa na kuhatarisha maisha ya takriban watu milioni 900 wanaoishi kwenye sehemu za nyanda za chini.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, Guterres ametoa ripoti ya kutisha ikiwa ya kwanza ya aina yake mbele ya baraza la usalama la UN kuhusu tishio la amani na usalama wa kimataifa kutokana na kuongezeka kwa maji ya bahari , akionya kwamba hali hilo itaendelea kushuhudiwa licha ya viwango vya ongezeko la joto kudhibitiwa kwenye degree 1.5 Celcius kuendana na malengo ya kimataifa.

Kando na mataifa aliyosema yapo hatarini, Guterres pia ametaja miji mikuu kadhaa ambayo ipo hatarini kama vile Cairo, Lagos, Maputo, Bangkok, Dhaka, Jakarta, Mumbai, Shanghai. Copenhagen, London. Los Angeles, New York, Buenos Aires na Santiago.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG